Majuto
Captain Smyzy

....yeah, thiz about life man.....(chiness bizness) Every thing you do, Fikiria, hujui place utaishia...au sio

verse 1

Skiza story yake, mwana wa mabepari

toka alipozaliwa hali yake ilikuwa shwari

kama mtoto yeyote aliishi na wazazi

na alipotak chochote alitegemea wazazi

hizo hela za babake zilimpa ujeuri

hakuna mtu yeyote aloweza kumshauri

wote aliwachukua tu kama watu mabwege

bila kujua hatimaye hali yake itakuwaje

wazazi walimpenda mshkaji kaanza kudeka

kajiona ameshafaulu shuleni akatoweka

kajiunga na vikundi haram wakamchombeza

mi nashindwa kwani hakufaham watampoteza?

mshkaji alizidisha vituko kila kukicha

leo kaiba mbuzi kesh okuku kamficha

kapelekwa kwa chief, ili apate kumkashif,

hapo bado kaishia kumtongoza mke wa chifu.

Chorus

Nilimuonya lakini hakusikia

aliona kama mimi siwezi kumsaidia

cheki sasa hatimaye anajutia

vitu alivofanya ndo sa' vinamchukia x2

verse 2

Zilipita siku chache hali ikizidi kuwa mbaya

bwana chifu kampitisha kwenye koti za wilaya

mateso aloyapata siwez kusimulia

na mpaka siku ya leo bado nazifikiria

alifanywa atembee huku amefungwa miguu

wakamweka kwenye celi akisubiri siku kuu

back at home, watu walishachoka naye

mpaka wazazi wake walishachoka kuishi naye

siku ilipowadia alipelekwa mahakamani

kesi yake iliposikizwa alihukumiwa maishani

cheki sasa anajuta, nafsi inamsuta

kwani yeye ndo chanzo kwa yale yote yalomkuta

sina uwezo wowote mie wa kumsaidia

nilimuonya mara mia kaniona kama gunia

so, peace for life, namalizia story yangu

asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu.

chorus x2


  Purchase "Majuto"   Purchase Entire Album   Email Video to Friends   Play Youtube "Majuto" Video   Play Spotify "Majuto" Song   View Wikipedia "Majuto" Entry   Receive Emails for Future Captain Smyzy Lyrics

Email:

  Link to "Majuto"   Share on Facebook, Twitter, and more
  See Recommended Lyrics For You

Loading...

Lyrics by Captain Smyzy

Related Songs