Nitafanya
Kidum

Verse 1(Kidum)

Ikiwa umeamua kunitoroka

ikiwa unahisi hujiskii nami tena

na mbona imekuwa ngumu kunidokeza

naona ni bora nilie leo, badala ya kesho

kupenda, usipende

ni kama kujitia kitanzi

nitachimba na sururu

kwa ardhi nikitafuta penzi lako

ni heri nipigwe fimbo kwa mwili

sababu ntajikuna ama ntajikanda na maji moto

maumivu ya penzi, mtu hajikuni

wala hajikandi na maji

na hakuna upasuaji

Chorus

kama

kuna kosa nimewahi fanya(nielezee)

kama

kuna jinsi tunaweza leta(mpaka niishi)

na kama

kuna kitendo linaweza tendwa(nielezee)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

Verse 2(Lady Jay Dee)

kweli hukumbuki ulioyafanya

ni kweli unakumbuka tulikotoka

sisemi habari zozote za kusikia

bali kwa ushahidi niliouona

msamaha mara ngapi

umeshaomba na bado

chenye makosa mangapi

niliyoyafumbia macho

mpaka leo nahisi kufika kikomo

maumivu yanazidi

ndani ya moyo

sitaki kwenda mbali kwani uko moyoni

nikusamehe mimi mara ngapi wee

nielezee mpenzi mara ngapi

Chorus

unataka nikusamehe mara ngapi(usihesabu)

ungependa nikuvumilie mara ngapi(hii ni ya mwisho)

je wewe nikulilie mara ngapi(vumilia)

sitoweza(utaweza wee)

nimechoka(usichoke)

nimeshindwa(usishindwe)

naondoka(usiondoke)

sitoweza(utaweza yee)

nimechoka

nimeshindwa(usishindwe)

naondoka(usishindwe)

Verse 3

ukihesabu mara ngapi umenisamehe

ni kama kuhesabu

ni mara ngapi mtoto kaharibu nappy

usichoke

usiondoke

usilie

niko hapa kukulinda

Chorus

kama

kuna kosa nimewahi fanya(nielezee)

kama

kuna jinsi tunaweza leta(mpaka niishi)

na kama

kuna kitendo lingeweza tendwa(nielezee)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

nitafanya(fanya)

nitatenda(tenda)

unataka nikusamehe mara ngapi(usihesabu)

ungependa nikuvumilie mara ngapi(hii ni ya mwisho)

je wewe nikulilie mara ngapi(vumilia)

sitoweza(utaweza wee)

nimechoka(usichoke)

nimeshindwa(usishindwe)

naondoka(usiondoke)

sitoweza(utaweza yee)

nimechoka

nimeshindwa(usishindwe)

naondoka(usishindwe)


  Purchase "Nitafanya"   Purchase Entire Album   Email Video to Friends   Play Youtube "Nitafanya" Video   Play Spotify "Nitafanya" Song   View Wikipedia "Nitafanya" Entry   Receive Emails for Future Kidum Lyrics

Email:

  Link to "Nitafanya"   Share on Facebook, Twitter, and more
  See Recommended Lyrics For You

Loading...

Lyrics by Kidum

Related Songs